Monday, October 18, 2010

Mhe.Angela Kizigha akihutubia kawe

MHE.DR.JAKAYA MRISHO KIKWETE AITEKA KAWE.DAR

Mhe.Dr.Jakaya Mrisho akihutubia kawe, awaomba wananchi kuichagua CCM kwa kuwa iliahidi na ikatekeleza.katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers huko Kawe.
Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Kawe Mhe.Angela Charles Kizigha katika mkutano wake wa kampeni uliofanyika viwanja vya Tanganyika Packers huko Kawe.
Mhe.Angela Charles Kizigha akiwaomba ridhaa Wananchi wa Jimbo la kawe kukichagua chama cha Mapinduzi , pia aliwaambia Wananchi watakapo mchagua atajenga hospital kwa ajili ya jimbo hilo, akitoa mfano kwa mbunge iddi Azzan anayo Hospitali ya Mwananyamala ipo katika Jimbo lake la Kinondoni, kwa hiyo na yeye atajenga ili kuipunguzia mzigo Hospitali hiyo.
Mhe.Dr.Jakaya Mrisho Kikwete akimnadi Bw. Othman, Mgombea Udiwani wa kata ya kawe kwa niaba ya madiwani wote wa Jimbo hilo la Kawe.
JK akijiandaa kumkabidhi Mh. Fatma Maghimbi kadi ya CCM baada ya kutangaza kujiengua chama cha wananchi CUF katika mkutano wa kampeni katika viwanja vya Tanganyika Packers vya Kawe.
JK akimkabidhi kadi ya CCM Mh. Juma Othman Juma
ambaye pia alitangaza kujiengua CUF
Wah. Juma Othman Juma na Fatma Maghimbi wakifurahia kujiunga na CCM.
JK akiongea na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam Mh. John Guninita, Mwenyekiti wa kampeni wa CCM Mh Abdulrahman Kinana na wasaidizi wake wengine
Mhe.Angela Kizigha akisalimiana na baadhi ya wagombea waliohudhuria mkutano huo, akiwemo Mhe.Iddi Azzan Mgombea Ubunge Jimbo la Kinondoni (kulia kwenye Picha)
Mhe.Angela Kizigha akizungumza kitu na Mgombea Udiwani wa kata ya Makumbusho Ndugu. Mutayoba.(Kusho kwenye Picha).
Mhe.Angela Kizigha akiwa katikati ya kundi la watu baada ya Mkutano kumalizika.
Watu walikuwa Nyomi hapatoshi.
Msanii Diamond akiburudisha umati huo
Vijana machachari wa Tip Top Connection wakifanya vitu vyao leo Kawe

Friday, October 15, 2010

MGOMBEA MWENZA URAIS WA CCM DR BILAL AKIHITIMISHA WIKI YA UWT PAMOJA NA KUWANADI WAGOMBEA UBUNGE NA UDIWANI WA WILAYA KINONDONI, DAR-ES-SALAAM

Mgombea mwenza Dr. Mohammed Gharib Bilali alihitimisha wiki ya UWT katika viwanja vya Mwinjuma kata ya Makumbusho, Kinondoni.alisema Chama Cha Mapinduzi kinajivunia umoja huo wa UWT kwani ni moja ya nguzo imara katika chama hicho.


Pia aliupongeza umoja huo kwa juhudi kubwa ya kuwakomboa wakinamama, na kuhakikisha wakinamama wanapata maendeleo na huduma zote muhimu, moja ya huduma hizo ni kupata mikopo yenye masharti ya unafuu zaidi. Na alimpongeza Mh. Jakaya Mrisho kikwete kwa kufungua benki ya wakinamama ili iwasaidie kwa maendeleo yao na kulisimamia taifa lao kwa uzuri zaidi.

Mwisho alimuombea kura Mgombea Urais Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na kuwanadi wagombea Ubunge wote wa wilaya ya kinondoni pamoja na madiwani.
Dr. Mohammed Gharib Bilali akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kawe Mh. Angela Kizigha katika uwanja wa mkutano wa wiki ya wanawake UWT uliofanyika kinondoni uwanja wa Mwinjuma.
Dr. Mohammed Gharib Bilal akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kinondoni Mh. Iddi Azzan wakati wa kuhitimisha wiki ya UWT.
Mgombea Ubunge Jimbo la Ubungo Mh. Hawa Ngumbi akinadiwa na Dr Mohammed Gharib Bilali katika wiki ya wanawake ya UWT.
Ndugu Leila Seif ambaye alikuwa Mjumbe wa baraza la wanawake Taifa kupitia Chama cha CUF arudisha kadi CCM kwa Mheshimiwa Dr. Mohammed Gharib Bilal. wakati wa mkutano wa UWT, uliofanyika viwanja vya Mwinjuma, Kinondoni.